Luke 23:1-5

Isa Apelekwa Kwa Pilato

(Mathayo 27:1-14; Marko 15:1-5; Yohana 18:28-38)

1 aKisha umati wote wa watu ukainuka na kumpeleka Isa kwa Pilato. 2 bNao wakaanza kumshtaki wakisema: “Tumemwona huyu mtu akipotosha taifa letu, akiwazuia watu wasilipe kodi kwa Kaisari na kujiita kuwa yeye ni Al-Masihi,
Al-Masihi maana yake ni Masiya , yaani Aliyetiwa mafuta.
mfalme.”

3 dBasi Pilato akamuuliza Isa, “Wewe ndiye mfalme wa Wayahudi?”

Isa akajibu, “Wewe wasema.”

4 ePilato akawaambia viongozi wa makuhani na watu wote waliokuwepo, “Sioni sababu ya kutosha kumshtaki mtu huyu!”

5 fLakini wao wakakazana kusema, “Anawachochea watu kwa mafundisho yake katika Uyahudi yote, tangu Galilaya alikoanzia, hadi sehemu hii!”

Isa Apelekwa Kwa Herode

Copyright information for SwhKC